BIASHARA YA CHUPI{vifuniko vya Asali} Ni biashara yenye faida kubwa ikiwa umepata eneo lenye mzunguko mkubwa wa fedha na mkusanyiko wa watu vitu vya kuzingatia kuanza biashara hii ni kama vifuatavyo @bajabiri @mpambazi
Aina za chupi
Chupi zipo za ubora tofauti kulingana na material. Kuanzia za dzn Tsh 8,000 hadi Tsh 45,000 na kuendelea.
Kundi la dzn 8,000 hadi 14,000 tunaliita lonya, ni zile nyepesi (za watu wa kipato cha chini), 15,000 hadi 32,000 ni ubora wa kati (za wa kipato cha kati)
na 34,000 na kuendelea ni high quality (hizi za wa kipato cha juu).

Jua aina ya wateja wako ujue kundi gani la ubora ulangue zaidi. Si mbaya kuchanganya ila isiwe nusu lonya na nusu high quality. Kama wateja uliowalenga ni wa kipato cha chini basi jaza lonya na quality chache,
na kinyume chake ni kweli (vice versa is true).
Mtaji kiasi gani?
Inategemea na quality ya chupi uliyoamua kuuza. Mil 2 hadi 3 inaweza kukupa dzn 150 hadi dzn 200 za lonya, huku fedha hiyo hiyo ikakupa dzn 50 hadi 60 ya zile quality. Mtaji unaamuliwa na aina ya mzigo kulingana na wateja wako.
Size na aina ya wateja.
Kulingana na mahali unapoenda kuuza ila kumbuka wanunua chupi zaidi ni wadada wa rika la kati, umri miaka 20 hadi 32 Wengi hawana majukumu mengi ya kimaisha wanajipenda na wako kwenye mahusiano ya mapenzi motomoto. So, size za kundi hili ndizo ziwe nyingi
Wapi utapata mzigo wa jumla?
1. Dsm, Kariakoo mtaa wa Msimbazi na muhonda zipo lonya nyingi sana.

2. Dsm, Kariakoo mtaa wa mchikichini na Manyema (kama sijakosea majina) jirani na ukumbi wa ddc. Hapo kuna quality nyingi. Pia yapo maduka machache kule Congo, mtaa wa Mchikichi na
Nyamwezi, n.k
3. Mwanza pembeni ya njia panda ya barabara ya Pamba na Miti mirefu. Upande wa stand ya zamani ya Tanganyika. Maduka yako bondeni kidogo (yamejificha). @MiriamMkanaka
4. Kampala, Uganda kuanzia makutano ya William street na Ben Kiwanuka Rd, na ukiteremka na hiyo Ben Kiwanuka hadi unakaribia njia panda ya stend ya zamani ya daladala (Kampala Old Tax park). Kabla ya hiyo njia panda kuna maduka yako ndani ndani. @FarajaNyalandu
Kumbuka; maduka mengi ya barabarani hapo William street na Kikuubo Rd (tamka Chikuubo) yenye wauzaji wengi ni ya rejareja, maduka ya jumla yako ndani. YbKampala duka 1 wanaweza changia watu hata 6, kila mtu anauza upande wake. So, ukiona duka la nje limejaa na lina wauzaji wengi
Kuwa makini, wakijua ni mgeni nao wanajifanya wanauza jumla, then unapunguziwa kidogo kwenye bei yao ya rejareja so unakuwa umepigwa. @chapo255
Zingatia;

* Dsm unapata mzigo wa aina zote kwa bei nzuri
* Mwanza mzigo mwingi ni ile quality ya kati na unatoka Kampala na Nairobi. Nairobi zinatoka Skin tight na brazia nzuri na baadhi hazipo Dar. @BarakaSaimon3
* Bei za Mwanza ni juu kidogo kuliko Dar japo baadhi ya tight na brazia Mwanza ni nafuu na nzuri kuliko za Dar.
* Kampala chupi nyingi ni quality ya kati (si lonya wala high quality) na nafuu. Tatizo hawana brazia nzuri na tight nzuri.
Muuzaji
Kwa uzoefu wangu, wateja wengi hasa wadada (ambao ndio kundi kubwa) wanapenda wauzaji wa kiume hasa akiwa mchangamfu na mwenye kauli nzuri. Muuzaji asipitilize na kuleta utani na mitongozo.
* Wamama watu wazima sana hawapendelei wauzaji wa kiume ila endapo muuzaji akimpokea na kumsemesha kwa heshima, ananunua.
* Wanaume wanapenda wauzaji jinsi zote tu.
Akimkuta muuzaji wa kike atatamani ajue yeye anapenda ipi, akikuta wa kiume anatamani ampe uzoefu wanawake wengi wanachagua zipi. Hili nalo ni kundi dogo.
Ni chupi tu?
* Hapana, lazima uuze na skin tight, brazia, lesso, sox, night dress,vest, boxer n.k
* Biashara kuwa kijiwe cha story hadi kuziba wateja. Wadada wanaongea sana hasa ukiwachangamkia na wakikuzoea.
* Mteja kutaka kurudisha / kubadirisha nguo ya ndani baada ya kufika nayo nyumbani.
* Usikubali. Bora anune umpoteze coz hata ukimkubalia utampoteza pia coz atajua ndio mchezo wako.

* Kumbuka kutoa zawadi kwa wale wateja wa siku zote na kwa wale wanaonunua mzigo mkubwa. Mf.Kanunua chupi 8 @ Tsh 3000 - Tsh 4000. Mpe hata lesso ya 500. Haitokufilisi ila atafurahi
kumbuka biashara hii hata ukiwa mtandaoni unaweza kuifanya kujenga brand then ukaja fungua goli sio lazima uwe na goli tumia akili maarifa mitandao ya kijamii ni kama mitaa utategemea na unakaa mitaa gani pia mitandao ya kijamii traffick inauzwa kama bidhaa tuu @GillsaInt
Source kutoka kwa mdau mmoja uko JF
You can follow @ngomekombo25.
Tip: mention @twtextapp on a Twitter thread with the keyword “unroll” to get a link to it.

Latest Threads Unrolled: