"MALIPO HUWA HAPA👇 HAPA👇.."

Nilikua natetemeka,nahisi jasho linanitoka ila sioni kama linadondoka, jua limenipiga ila ndani nahisi baridi..tumbo linaruka kama lenye njaa..kupumua nashindwa kama mtu mwenye pumu..meno yanagongana.. miguu imekufa ganzi..natamani kutapika..
Nikaachia kitasa cha mlango,nikageuka kuegemea ukuta..nikajikuta nimeteleza hadi chini..
Nakumbuka kwa mbali ZIGO remix ya @AyTanzania na @diamondplatnumz ilikua inakita kwenye speaker zangu..
Niliwaza nasikiaga tu kumbe ndo hivi inavyokuaga..
Mlango ukafunguliwa tena,akatoka mchizi wangu kabisa..kavaa jeans na vest mkanda una hang mabegani akachuchumaa nilipokua, kichwa kainamisha..akasema vitu ambvyo sikuvisikia..masikioni nasikia "zzzzzzz"
Alivyoona nimeduwaa akasimama na kuanza kuondoka..nilikaa pale kama nusu saa
Koo limenikauka..nikaamua niingie chumbani..
Nakuta manzi yngu ndani ya khanga,inalia inavuta tu kamasi..
Kwakweli sikuelewa kwann analia..
Jina langu likaanza kuitwa,maelezo na maombi ya msamaha yakatolewa kwa wingi huku ananisogelea ila akiogopa kuja karibu..na bora hakusogea
Nikaangalia jinsi alivyokua pini,tena ndani ya khanga ile..in short mpaka kipind hcho sikuwahi kupata manzi mkali sana kama yeye..
Moyo ukaacha kufunction kwa sekunde,akili ikachukua usukani..
Nikatamka "kwakua sijakuoa Natoka,Nsikukute, na ilo shuka ondoka nalo" af nkasepa
Nikasepa kwa mchizi wangu Sharif nikala,tukapiga FIFA sikueleza chochote..nilivyorudi kweli nikakuta maagizo niliyofanya yametekelezwa..
Ila simu yngu haikupumzka kwa text na calls zilizokua zinaingia..kama notification za uzi zinavyomiminikaga.
Siku,wiki hadi mwezi ukaisha..baada ya miezi miwili mlango ukagongwa mida kma ya saa moja usiku..nafungua ni yeye..akaniomba nimsikilize,bila hiyana nikakubali.
Alinambia alikua na mimba ya mchzi na mwana kaikataa,hajui cha kufnya..
Hawezi kwenda kwao,hajui kama abaki nayo au aitoe..hawez kuihudumia peke yake
Nilitamani kumsaidia cz bado nilikua namwelewa kichzi ila kama Noorah nikamwambia "Sina cha kukusaidia labda tu nikusaidie kumchagulia jina"
Akaanza kulia..ila ndo hivyo moyo wangu ulishaamua
Ulipita muda mrefu sana kiasi cha kuanza kumsahau hadi wiki chacge zilizopta nilikutana na rafiki ake na katika stori moja mbili akagusia kuhusu huyo X wangu..kua manzi aliacha na kusoma..kwao walimsusa kweli na kibaya mimba ilitoka,hali si shwari,yupo yupo tu.
Nikachukua namba yake ya simu,ila bado najiulizaga kama nimtafute au vipi!?bado sijafanya maamuzi..
Alinitenda vibaya ila naona kama nshamsamehe..ila nahisi nikimsaka mengi yanaweza ibuka maana viporo mara nyingi huishia kupashwa..
Oooh na yule mchizi wangu siku nipo whatsapp group la wana wangu inatumwa video jamaa kaingia choo cha kike kafumaniwa tena na alichofanywa sio poa..najua mnajua...na uhakika wengi wenu mshaionaga maana ilitrend kweli.
Nilimwonea huruma na ilinisikitisha ila ntakua mnafiki kama sitasema moyoni kidgo 'nilifurah'..

Leo sitafoka..😆

Ila mwendelee kuwa na Eid Mubaraak njema.
Endeleeni kuwa nami kifikra..✌

#fanani✍️ hapa
https://twitter.com/MwebeKelvin/status/1256952328034418689?s=19
You can follow @crazyTanzanian.
Tip: mention @twtextapp on a Twitter thread with the keyword “unroll” to get a link to it.

Latest Threads Unrolled: