Acha Leo tumcheki mwenetu Willie Junior Maxwell II a.k.a Fetty Wap

Tumuangalie kwa uchache sana,Kwanini muonekano wake wa macho uko vile,

Jina la Fetty Wap lilitokea wapi,

Mafanikio ya Ngoma ya Trap Queen na tutajua sababu ya yeye kukaa kimya kwenye Game
Jina Fetty Wap sio geni kabisa masikioni mwako haswa kwa machizi

Fetty Wap kwanza kabisa alizaliwa mwaka 1991 pale New Jersey

Hapa alizaliwa akiwa mzima kabisa yani macho yake yalikua sawa
Katika moja ya interview yake ya mwaka 2015 aliweza kueleza wazi nini sababu ya yeye kua vile

Yani Jicho lake kupata ile shida
Anasema wakati akiwa mdogo alikua poa ila alipata Glaucoma huu nadhani ni ugonjwa wa macho na anahisi alizaliwa nao ila
Ulikuja kumletea tabu yani akaanza kuumwa na macho anasema anawashukuru sana madaktari

Kwa kuweza kumsaidia Jicho lake moja kuona maana Jicho lingine walishindwa

Badala yake alipewa Ocular Prosthesis atumie

Aah tumeshajua mchizi ule ni ugonjwa sio ajali kama Madai ya
Vijiweni

Turudi sasa mwaka 2013 hapa Fetty wap alikua na kiu ya kufanya mziki na alisema alitaka Afanye kitu tofauti sana kwenye game

Hapa alikua Anaitwa Fetty yani wanae wakimaanisha Money mchizi alikua mtafutaji pesa sana

Alikua anaimba ila hakupata nafasi
Wanasema kufanikiwa ni siku moja kuna siku kulikua na show ambayo lengo lake lilikua kumchangia rapper Gucci Mane

Kwa matatizo yaliyomkuta mchizi akaenda sasa wakati anaandikisha jina aliandikisha Fetty ila muda wa kutajwa apande kwa stage

Anashangaa jina linakuja Fetty Wap
Yani wahuni wakaongezea mafekeche mchizi akashanga hii Wap imetoka wapi

Kama utani jina likashika mpaka leo
Mwaka 2014 alitoa ngoma Kubwa sana

Hapa wahuni lazima waelewe Naposema ngoma kubwa hii si nyingine ni Trap Queen

Sasa hii ngoma ilitoka Feb lakini cha ajabu
Ikabuma mpaka November ikaamsha upyaa kivipi kwanza

ilikua played pale SoundCloud Mara 130mil ikachukua platinum chap

Mchizi akaingiaa kwenye XXL Freshman Class ya mwaka 2015 hii ni trap queen mzee inamfungulia milango

Hii ngoma ilikua ngoma kubwa sana usibishe
Alivunja rec ya Tunechi ya mwaka 2011 aliyoweka ya 1St Male in 4yrs concurrent single reach the top 10

Tusisahau sep 24 2015 alitoa album yake ya kwanza iliyoitwa Fetty Wap ikiwa na mikwaju kama 679,My Way,Again

Ila Trap queen ilizibeba ngoma zote
Grammy ilichukua kama best rap song sawa

iHeartRadio awards waliipa kama Hip Hop song of the year na mchizi akawa kama Hip Hop artist of the year hii ni 2015

2016 billboards award mchizi akachukua kama Top rap artist na ngoma ilichukua kama top stream song

BET wakaipa kama
Best Club Banger na people champ choice haya ni mafanikio tu Trap Queen

Pia alionekana kwenye collabo na Fifth Harmony ngoma ya Flex All in my head,promises ya Kid ink 2016

album pamoja na Ep zake

Bruce Wayne 2018,King Zoo,For my fans pamoja na Trap & B
Hii Ep ameitoa 14Feb 2020

Japo haikupokelewa vizuri tofauti na kazi zake za hapo nyuma

Twende kwanini mchizi amekua kimya hivo tunajua mchizi wakati anaingia kwenye game alikua chini ya 300 pamoja 1738 seventeen thirty eight

Na kazi zake nyingi zilikua pale ila sasa
Alikuja kusign deal na Atlantic rec kitu ambacho 300 walipishana

Nadhani kuna namna walipishana yani mchizi nadhani alisign contract Mara mbili

Sasa hapa ikawa tabu kazi zake 300 ikawa shida kuziachia japo kazi zilikua zinatoka pia muda msingi mchizi alikua mahakamani
Kuna siku 50 cent aliwahi kusema kwamba uongozi wa Fetty Wap ndio unafanya ukimya wa mchizi

Yani wanasumbua akiwalenga 300 mchizi yupo na Ana kazi ila sasa anatakiwa amalizane na three hundred 300

Pili Ana mambo ya kifamilia pia yanachagiza
Mchizi mpaka sasa Ana watoto 6 na amezaa na wanawake tofauti

Alipotisha zaidi ni pale alipozaa na mwanadada Masika Kalyishia kama unafatilia TV series ya Love & Hip Hop Hollywood

Utakua Unamjua sana hapa kama unaangalia hawavumi lakini wamo au sijui kapuni my friend Itakua
Ngumu

pia alishawahi kuonekana katika baadhi ya Ep kwenye msimu wa 6 nadhani kabla hawajatengana na Masika

Kiasili Fetty Wap ni mtu wa Haiti kule kwa kina 21 Savage

Alishawahi kusema kua Haiti ina maana Kubwa sana kwake na hupendelea kutoa misaada kwa families
Zisizojiweza pia hupeleka misaada kule hospital kwa wale watoto wenye wanaugua Maradhi kama yake

Juzi niliona mke wake amemfungulia case akitaka apewe talaka yake ila aliongea shit sana

Alisema maisha yao yalikua ya Pombe na drugs pia alikua anapigwa
Jambo ambalo Fetty wap alikanusha na kusema sio kweli kwa sisi wataalam

Hii Mbinu aliotumia Huyo mke wake ni kwa sababu anataka case yake iwahi kusikilizwa na talaka itoke Mara moja

Baadhi ya marafiki wa Fetty Wap walisema mchizi Hana tabia ya kupiga wanawake kabisa
Sasa kitu kimoja nilichopenda kwa mchizi ile Ocular prosthesis mchizi haivaagi kabisa

Anataka kua real ndio maana Jicho lake huonekana jeupe kabisa mpaka Unaweza kusema jamaa kakosa ela au

Vipi kama wengine wanavofanya kwa kuogopa kuonekana tofauti kwa jamii
Yeye hilo hajali anasema yeye ni real anajikubali

Rapper Gucci Mane ndio aliemfanya akaingia kwenye Game yani huyu ndio aliemu influence

Kama alivofanya pia kwa 21 Savage hivo bhasi Gucci Mane tuappreciate mchango wake kwenye Game.

#CelebrityLifeStyle
#TillerBrief
You can follow @TillertheWorld.
Tip: mention @twtextapp on a Twitter thread with the keyword “unroll” to get a link to it.

Latest Threads Unrolled: