THE PAINFUL SECRETS BEHIND HER BEAUTIFUL SMILE πŸ’”

Dear fam,
Moyo hauna kioo kusema utaweza chungulia ukaona ya ndani.Moyo wa mtu ni kama giza totoro mbele ya kipofu. kila mtu ana magumu anayopitia japo si rahisi kutambua.

Hakustahili kuyapitia yale yalomkutaπŸ˜–

T H R E A D πŸ‘‡
Tabasamu la mtu huficha mengi yalojaa rohoni na fukuto zito la tabu,shida,sonona na mahangaiko moyoni. Tunachozidiana ni jinsi ya kumudu kuonesha hayo mbele za watu.
My story began a way back nlipomaliza darasa la saba ambapo ilitakiwa nikajiunge na kidato cha kwanza kwenye
Shule moja pale Morogoro. Kutoka mikoani huko ile shule niliposoma nilikua peke angu tuu niliyefanikiwa kufaulia shule za nje ya mkoa kati ya wale wanafunzi kwenye lile darasa.πŸ˜„
Furaha ilikua kubwa kwa sifa nyingi kutoka kwa ndugu na marafiki mpaka ilipoingia huzuni siku
Naagwa kuelekea shule..Ile kusindikizwa stand na ndugu na marafiki ni kitu kichungu sana. Goodbyes always hurtπŸ’”

Mbaya zaidi mzee alinambia nijipeleke mwenyewe kuanza form one kwa madai mi ni mwanaume siezi potea na ukizingatia ndo ilikua mara ya kwanza kutoka nje ya mkoaπŸ˜’
Bimkubwa alikataa lakini mwisho hakua na namna so akaniandalia kuku na chapati zisizoharibika zinisitiri njiani..Ila wamama wapo na upendo nyie πŸ™ŒπŸΌ

Ye alichofanya baba ni kuninunulia simu aina ya Vodafone zile za promotion akanijazia na vocha tuwe tunawasiliana πŸ˜‚
Nkasema fresh
Safari ikaanza mpaka Moro town Stand ya Msamvu bana. Nkashuka kuchukua mizigo kwenye buti,sasa ile kuhamaki basi limeshaondoka (maana lilikua linaendelea mpaka Dsm)
Nkakumbuka begi langu dogo lililokua na simu na pesa zote za matumizi nimelisahau kwenye gari na gari limeondoka😨
Nkahisi kizunguzungu nkiangalia ilitakiwa niendelee na safari mpaka huko kwenye moja ya Wilaya za Morogoro ambapo ndipo shule yangu ilipo 😫
Nkiangalia saa ni saa 17;30 na sijui huko ntatumia muda gani kufika Ili niunganishe mpaka shule tuu maana hela ya kulala guest sina tena
Mungu mwema nkajisearch mfukoni nkakuta na 10k nkatafuta basi lakuelekea nakoenda nkalipia 6k.
Nikakaa kusubiri gari liende na safari ikaanza rasmi 18;00 Jioni kabisa.Pembeni yangu alikua amesimama mama mmoja wa makamo ya 42yrs mzuri kiukweli japo alionekana kachoka kweli
Licha ya kuwa nauchovu wa safari za kuunganisha lakini nkamuomba yule mama aje akae nilipokua nimekaa mimi nisimame, maana nakumbuka maneno ya mama Noe kabla ya safari alinambia niheshimu kila mtu sasa nkaona isiwe tabu nianze kuishi maneno ya mama πŸ€—

Yule mama akakaa tukaenda
Aisee nilisimama mpaka nkasimama tena,magoti nyonga vyote vinauma hatimae tulifika mida ya saa nne usiku 😀
Nikashuka lakini sielewi nianzie wapi nimalizie wapi. Nkaona nimuulize yule mama kuhusu mahali shule yangu ilipo. Alinionea huruma sana kabla hata sijamwambia yalonikuta
Akasema " Mwanangu umechoka sana, twende kwangu ukapumzike halafu kesho ndio uende huko shuleni "
Nkaona poa tuu liwalo na liwe hata kama ni wachuna ngozi maana ndo story zilizokuwepo by then πŸ˜‚
Akanichukua mpaka kwake..Aliishi pazuri kiukweli lakini sikukuta mtu mule ndani
Nkamuuliza kama anaishi mwenyewe akasema anaishi na Mumewe.
Tukala chakula nikaoneshwa chumba kulikua na kila kitu so nkaoga nkalala. Sasa usiku katikati ya usingizi nkahisi naota kama kuna sauti za watu wanapigana yani ile kama mwanaume anamfokea na kumpiga mwanamke dooh!!
Kustuka kumbe ni kweli asee yule mama alikua anapigwa sana na mumewe ule usiku. Nilijiskia vibaya maana kwa hali ya uchovu aliokua nao halafu akutane na kipigo tena πŸ’”
Nlikua na umri mdogo jumlisha ugeni nisingeweza kusaidia chochote zaidi ya kukaa naskia mwanamke akiugulia
Asubuhi ikafika nkaamka nkamkuta yule mama yupo anaandaa chai. Alivoniona akatabasamu sana na uso wake ulovimba, ile taswira siwezi isahau.
Nkamuuliza akanambia alijigonga mlangoni alipokua anaamkaπŸ˜’. Nkapotezea tukaendelea na story zaidi ndipo nkamsimulia yalonikuta mpaka
Kuibiwa. Maana hadi wakati ule nyumbani hawajui nimefika au laah na kwa jinsi navyomjua mama nahisi alikua ameshalia mpaka kachokaπŸ˜„.
So baada ya kumsimulia yule mama alinihurumia akaniahidi nikae pale mpaka atakapopata hela ili anipeleke shuleni. Sikuamini macho yangu
Guys, watu wema bado wapoπŸ™ŒπŸΌ
Siku ikapita usiku ukaingia, akaja mwanaume ambae hakika nilihisi tuu atakua mume wa yule mama ambae baadae nilijua anaitwa mama Sele.
Yule mama akasimama kumpokea lakini akasukumwa mpaka chini,hapo nilistuka sana halafu yule mwanaume akaingia zake
Chumbani. Mama Sele akaamka anatabasamu kama vile hamna kilichotokea nkamuuliza " mama mbona ivi" akanijibu ati ni kawaida tuu mumewe kachoka na atatulia πŸ˜’
Nilizidi kuumia. Nilikua mdogo lakini nkagundua Domestic Violence is real.
Sasa bhana kama kesho kutwa yake usiku yule
Mwanaume akarudi amekasirika, mama Sele akanambia nikalale nadhani hakutaka nione kitakachojiri.
Zilizofata ni kelele na hofu kuu ya maumivu mwisho nkaskia" NA LEO HAULALI NDANI"... Iliniwazisha sana, inakuaje hivi? Mama Sele anakosa gani? Au mumewe ni mgonjwa?
Asubuhi sana nkaamka kwenda kufungua nkamkuta kalala kibarazani,nkamstua alivoamka akanambia aliamka mapema kufagia uwanja akajikuta amelala kisa uchovuπŸ˜’
Bhana chozi la utoto lilinitoka nkarudi ndani bila kuongea kitu. Mida ya mchana ikafika akanambia nijiandae nimsindikize
Mjini.Kweli tukaenda akanambia tunaenda akaninunulie mahitaji ya shule maana kuna hela zake za vikoba amepata. Njia nzima nilienda namuangalia mgongoni yawezakua ni Malaika na anamabawa kayaficha πŸ˜–β€

Baada ya manunuzi akaanza kunipa story kipindi tunarudi maana nilimuuliza
"mbona unaitwa mama Sele halafu Sele mwenyewe simuoni " ikabidi anambie kwamba yeye amekaa muda mrefu kwenye ndoa bila kupata mtoto na mpaka ilo jina la Sele ni la mumewe so wanamuita " Mama Sele
Hapo nkaunganisha dots anhaa yawezakua hata kile kipigo cha mumewe ni sababu hii πŸ’”
Akaniomba kuanzia wakati ule niwe namuita MAMA ili ajiskie vizuri. Sikusita nkamuita "mama " akaitikia " Abee mwanangu" huku akitokwa machozi
Nilijikuta namuonea huruma pale aliponikumbatia mbele za watu akiendelea kulia.. Basi tulipofika home nkala chakula akanipeleka shule
Huyu mama yangu mpya..Akalipia michango yote nakuacha namba za simu ili likitokea tatizo atafutwe. Tukaagana ye akarudi zake nyumbani. πŸ’”
Nilimuombea sana yule mama. Kila weekend alikua anakuja kunitembelea shuleni na zawadi lukuki.
Sasa zikapita weekend kama mbili bila kuja
Kunitembelea nkaanza kupata wasiwasi na bahati nzuri mzee alinitumia barua iliyoambatana na pesa za matumizi kupitia sanduku la posta la shule hiyo ni baada ya kuona nipo kimya.
Shule zikafungwa ikabidi kesho yake niende kwa Mama Sele nimsalimie kabla sijaenda nyumbani.
Khee 😳
Nkakuta mwanamke mwingine..Kwenda kwa jirani kuuliza nkaambiwa mama Sele aliondoka muda mrefu karudi kwao Morogoro mjini.
Akantajia mtaa unaitwa Sabasaba akanitajia mpaka nyumba. Nkafanikiwa kufika kwao lakini majonzi ndipo yakazidi maana niliambiwa mama Sele alirudi nyumbani
Akiwa anaumwa maumivu makali ya kichwa na upande wa mbavu na baada ya kuchukuliwa vipimo ikaonekana mbavu moja ya upande wa kushoto imevunjika na kuna damu ilivujia kichwani
Madaktari wakathibitisha alikua amepigwa na vitu vizito.Cha ajabu alipoulizwa akadai alivamiwa na watu πŸ˜’
Juhudi za matibabu zilifeli na hatimae mama Sele alifariki dunia.Niliumia sana maana ile kwamba alivamiwa na kupigwa na watu sikuamini kabisa kwa sababu alitoka kwa mumewe na maisha aliyokua anaishi na mumewe dah πŸ™ŒπŸΌ
She kept her worst secret.Domestic violence is real guys
You can follow @Vet_doctor87.
Tip: mention @twtextapp on a Twitter thread with the keyword β€œunroll” to get a link to it.

Latest Threads Unrolled: