AN OPEN LETTER ๐Ÿ’Œ TO MY EX ๐Ÿ’”

Hello beautiful,
Natumai uko salama sana pengine zaidi ya hata tulivokua wote.Ulifanyika baraka kwangu ndo maana leo nakutumia salamu.Simaanishi kuna nachohitaji kwako La hasha

T H R E A D ๐Ÿ‘‡
Ulikuja kwangu kama ua la kijani la pekee kwenye jangwa lakini haikufaa kitu tukaachana.
Ulinipa faraja nikajiona wa thamani kama kijito pekee kinachotiririsha maji pale jangwani. Nachoshukuru Mungu ulinikosea wewe na wala sio mimi kukukosea wewe ๐Ÿ’”
Nakumbuka mengi tulofanya pamoja nkajiona nipo peke angu kwenye dunia iliyotulia lakini kumbe niko na wenzangu wengi kwenye dunia ndogo ya moyo wako.

Uliniumiza sana zaidi ya kunikera nachoshukuru Mungu mimi nilizaliwa na furaha tumbo moja nacheka. Nkakubali yaishe๐Ÿ˜„
Nakumbuka mapenzi yako ya kiFilipino ya mimi na wewe kutembea kwenye mvua but trust me sasaivi nimenunua mwavuli.

Haimaanishi nadharau kumbukumbu zile hapana sitaki kutembea kwenye mvua ili niumwe kifua nife wakati we upo unafurahia maisha na mtu wako mpya ๐Ÿ˜Ž
Dear Ex, kila nikivaa ile t-shirt ๐Ÿ‘• uliyoninunulia kama zawadi siku ya birthday yangu nakukumbuka sana natamani unione tena nikipendeza nayo mtaani.
Lakini pia natamani iishe haraka.Sio kwa ubaya, nataka tuu siku niifanyie dekio pale nyumbani ibaki kama kumbukumbu ๐Ÿ˜„
Ulikua mrembo sana.Ulinishawishi niache kushabikia muziki wa Diamond nimskilize Ali Kiba.Nliienjoy sana zile nyimbo tukiimba usiku.
Bahati mbaya mpaka hivi navoandika huu ujumbe kwako nipo naskiliza JEJE ya Diamond.Sio kwa ubaya ni vile nataka nisiwe sawa na bwana wako mpya๐Ÿค—
Dear Ex, nakumbuka sana tulivokua tunalala wote pale kitandani nikikukumbatia kila nikijigeuza.Nilifurahi sana

Ila kwa sasa nimenunua mito mitano ya kitandani ili niwe naikumbatia nilalapo.Haimaanishi nakulinganisha na mto hapana ni vile mito mitano ni mingi halafu we ni mmoja๐Ÿ˜‰
Mpendwa Ex ulinivunja moyo wangu ๐Ÿ’” nlikua Samson ukaamua kuniDelila.
Nakuombea huko uliko ufanikiwe maana we si adui yangu.Furaha yangu siku moja nikukute upo kitengoni na mimi ili nikija kwenye interview nipate kazi kwa urahisi.
Dear Ex, ulinichanganya sana maana ulisema unapenda mimi nawewe tukiwa tunatembea kwa miguu njia nzima lakini ukaja kuniacha ukaenda kwa jamaa mwenye gari.๐Ÿ˜’

Nachoshukuru hata mimi kwa sasa namiliki magari mengi sana japo yako kwenye game za simu tuu lakini my future is bright
Nakuombea upate watoto wazuri kama au zaidi yako wakike tupu kama wanne kwa mujibu wa uzazi wa mpango itapendeza.

Natamani pia niwe jirani yako huko mbele. Si kwa ubaya, nataka pia ukiwa na hao watoto wakike wanne na mimi huku niwe na wakiume wanne ๐Ÿค—
Picha zako kwa bahati mbaya zilipotea pamoja na simu ile niliyoibiwa. Ni miongoni mwa kitu kilichoniuma sana

Basi ukipata ujumbe huu naomba unitumie zile picha zako zote. Si kwa nia mbaya hapana, nataka ukintumia nizifute mwenyewe ๐Ÿ˜„
Ulikua mwanamke mzuri sana,tuliahidiana mengi pia.Nakumbuka uliniambia nikikuacha utakonda.Cha ajabu siku ile nimekutana nawewe unaenda kwa fundi kuongeza ukubwa wa nguo kwa jinsi ulivonenepa๐Ÿ˜ญ
Nachoshukuru na afya njema mpaka sasa. Bado sina hela kama ulivoniacha but am not poor am pre-rich.
wewe kwangu ni wa maana sana.Nakuomba tukikutana basi usisite kuniita tusalimiane japo zisizidi dakika tano maana picha ya ile siku nakufumania itanijia na sitaki kuozea jela๐Ÿ˜ซ
Zaidi ya yote mimi sijabadilika lakini sio yule Noe wa zamani.Kuna siku ntakupa lift na ntakupeleka kwa mumeo ukiwa ndani ya Range Rover wakati yeye IST yake ikiwa garage kakosa pesa ya kuitoa. Ex wako sio adui yako lakini sio lazima awe rafiki yako
#End
#MyMindSpeak
#NohTalk โ˜•๏ธ
You can follow @Vet_doctor87.
Tip: mention @twtextapp on a Twitter thread with the keyword โ€œunrollโ€ to get a link to it.

Latest Threads Unrolled: